Jumapili 21 Septemba 2025 - 11:41
Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Hawza/ Mufti wa Tanzania Sheikh Abuubakar Zubeir Ally Mbwana, aliandaliwa tafrija ndogo ambayo iliambatana na uzinduzi wa kitabu cha miaka kumi ya utumishi wake tangia kukabidhiwa kijiti cha kuendesha Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Mwakilishi wa mshauri maalum wa Mufti kutoka Dodoma Alhaj Salum Seja ambaye kwa niaba ya Mh. Mshauri Maalum wa Mufti Alhaj Ismail Dawood alimkabidhi mgeni Rasmi Mh. Waziri Abdallah Ulega, kitabu maalum cha miaka kumi ya Baraza Kuu la waislamu wa Tanzania na Mufti Sheikh, Abubakar Zubeir Ali Mbwana.

Uzinduzi huo umlifanyika BAKWATA makao Makuu kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka kumi ya Mufti ambayo ilihudhuria na wajumbe Baraza ya Ulamaa , Masheikh, makatibu wa BAKWATA mikoa yote nchini pamoja na viongozi wa taasisi zingine nchini.

Kitabu hicho chenye kurasa 513 kimeandikwa na Harith Nkussa, mwandishi Rasmi wa Mufti na kuchapwa na Victory Bookshop Dodoma.

Hafla hiyo ilikuwa ni uzinduzi wa Msimu wa kumbukumbu ulioanza tarehe 10.9.2025 (Mufti day)  mpaka kilele cha BAKWATA day December 17 2025.

Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Uzinduzi Rasmi wa Kitabu cha Miaka Kumi ya Mufti wa Tanzania Wafanyika

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha